Sunday, 7 August 2016

NEWS TIME

There was an error in this gadget

RAIS DKT. MAGUFULI ASALI KATIKA KANISA LA BIKIRA MARIA PAROKIA YA CHATO, PIA ATEMBELEA KANISA LA ANGLIKANA, AIC PAMOJA NA MSIKITI WA OMAR BIN-L-KHATTAB CHATO MKOANI GEITA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli wakisali katika ibada ya Jumapili katika Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na waamini wa kanisa Katoliki wa Parokia ya Chato mara baada ya Ibada katika kanisa hilo Chato Mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihamasisha mchango wa ujenzi wa Kanisa jipya la la Bikira Maria Parokia ya Chato mkoani Geita.




MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AWASILI MKOANI LINDI TAYARI KWA MAADHIMISHO YA KILELE CHA SIKU YA WAKULIMA NANENANE KESHO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewasili mjini Lindi mchana huu akitokea mkoa wa Dar es Salaam kwa njia ya barabara ambapo hapo kesho anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha   Sikukuu ya Wakulima Nanenane kitaifa kwenye viwanja wa Ngongo katika Manispaa ya Lindi.


Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufunga maonyesho hayo ya Nane nane hapo kesho kwa  niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta John Pombe Magufuli.


Alipowasili ikulu ndogo mjini Lindi Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan  amepokelewa na Mkuu wa mkoa wa LINDI Godfrey Zambi pamoja na Viongozi mbalimbali wa Serikali na wa vyama vya siasa.


Katika Msafara wake, Makamu wa Rais ameambatana na Waziri wa Kilimo, Maliasili na Uvuvi wa Zanzibar Mhe. Hamad Rashid.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mstahiki Meya wa Lindi mjini Ndugu Mohamed Liumbwe mara baada ya kuwasili mkoani Lindi
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akivishwa skafu wakati wa mapokezi na Vijana wa mkoa wa Lindi .(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Wakina Mama wa mkoa wa Lindi wakimuimbia nyimbo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa mapokezi mkoani hapo.
 Wakina Mama wa mkoa wa Lindi wakimuimbia nyimbo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa mapokezi mkoani hapo.

WAZIRI MKUU MAJALIWA USO KWA USO NA ASKOFU GWAJIMA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Askofu Josephat Gwajima wa Kanisa la Uzima na Ufufuo katika hafla ya harusi ya Naibu Waziri wa Sheria na Katiba Amon Mpanju na mkewe Analises iliyofanyiak kwenye ukumbi wa jeshi wa Lugalo jijini Dar es salaam Agosti 6, 2016.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba, Amon Mpanju akilishwa keki na mkewe , Analises katika tafrija ya harusi yao iliyofanyika kwenye ukumbi wa Jeshi Lugalo jijini Dar es salaam Agosti 6, 2016. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary walihudhuria katika tafrija hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba, Amon Mpanju akimlisha keki mkewe , Analises katika tafrija ya harusi yao iliyofanyika kwenye ukumbi wa Jeshi Lugalo jijini Dar es salaam Agosti 6, 2016. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary Walihudhuria katika tafrija hiyo.

WAKAZI WA MBEYA WANUFAIKA NA GULIO LA SIMU LA BEI CHEE ZA VODACOM TANZANIA

Mfanyakazi wa Vodacom Tanzania, Lawreny Vimenty(kulia) akimkabidhi John Mwalusako simu aliyonunua jana katika Gulio la simu linaendeshwa na kampuni hiyo, katika kituo cha mabasi cha nane nane wakati wa maadhimisho ya wakulima Nane nane yanayoendelea katika uwanja John Mwakangale jijini Mbeya.
Wacheza shoo wakiendelea kutoa burudani kwa wateja waliofika kwenye Gulio la simu lililoendeshwa na Vodacom Tanzania,katika kituo cha mabasi cha nane nane wakati wa maadhimisho ya wakulima Nane nane yanayoendelea katika uwanja John Mwakangale jijini Mbeya.
Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania(wenye flana nyeusi) wakitoa huduma mbalimbali kwa wateja waliofurika katika Gulio la simu liloandaliwa na kampuni hiyo,katika kituo cha mabasi cha Nane nane nje ya viwanja vya maonyesho ya wakulima Nane nane maarufu John Mwakangale.


BWAWA LA MAINI LILIVYOITANDIKA BILA HURUMA TIMU YA DUNIA MABAO 4-0 KATIKA DIMBA LA WEMBLEY

Ulikuwa usiku mujarabu kwa vijana wa Jurgen Klopp, Liverpool ndani ya dimba la Taifa la Ungereza,Wembley baada ya kuisambaratisha bila huruma bingwa wa Laliga Barcelona kwa mabao 4-0 na kuwaacha mashabiki wengi wa soka Ulimwenguni wasiamini walichokiona na kukisikia.

Wakicheza kwa kujituma huku wakifahamu wazi kuwa wanacheza na timu bora kabisa duniani, wachezaji wa Liverpool walihakikisha hawawapi nafasi wapinzani wao kumiliki mpira kwa kuingilia pasi zao,dakika ya 14, Lalana anamnyang'anya mpira Alex Vidal na kumpa pasi Firmino ambaye anamrudishia Lalana naye anampa tena Sadio Mane na bila ajizi anaukwamisha mpira huo wavuni,1-0.

Goli hilo linadumu hadi mapumziko, kipinndi cha pili kilipoanza inachukuwa dakika moja tu Liverpool wanaandika bao la pili kwa beki Mascherano kujifunga akiwa katika harakati za kuokoa mpira uliopigwa na Sadio Mane. 

Dakika moja baadaye yaani dakika ya 47, Stewart anampokonya mpira Busquets na kumpenyezea pasi murua Diovick Origi anayewazidi mbio Gerard Pique na Mascherano nakupiga shuti linalopita katikati ya miguu (tobo) ya kipa wa Barcelona Terstegen. 3-0.

Katika kipindi hiki timu zote zilifanya mabadiliko ya wachezaji zaidi ya 6 kwa kila timu, na hapo Barcelona walitawala zaidi mpira na kufanya mashambulizi mengi langoni mwa Liverpool lakini ngome ya Liverpool ambayo iliongozwa na Lovren ilicheza kwa nidhamu ya hali ya juu na kufanikiwa kuzuia hatari zote.

Watu wakiamini kuwa mchezo unamalizika kwa hayo mabao matatu, Dakika ya 92 yaani dakika moja kabla ya mpira kumalizika kwa zile dakika za nyongeza Liverpool wanapora mpira katikati ya uwanja na kufanya shambulizi la kushitukiza, ambapo mpira wa krosi unapigwa na Markovic unatua kichwani kwa Grujic na kuupiga pembeni juu ya kona ya goli, waswahili hupenda kuita "anapotagia ndege" na mpira huo kutinga wavuni na kuandika bao la nne, hivyo kuhitimisha karamu hiyo ya mabao.4-0.

MASHINDANO YA MPINGA CUP 2016 KUANZA KUTIMUA VUMBI AGOSTI 12


MASHINDANO YA MAJESHI KUFUNGULIWA RASMI KESHO NCHINI RWANDA, JWTZ WAWASILI SALAMA MJINI KIGALI

Na Selemani Semunyu, JWTZ

Timu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzani limewasili Salama katika Mji wa Kigali Nchini Rwanda kuungana na Wanajeshi wa Nchi Za Afrika Masahariki katika Mashindano ya majeshi kwa nchi hizo yanayotajiwa kufunguliwa Rasmi kesho.

Kiongozi wa Msafara wa Timu hiyo Brigedia Jenerali Jairos Mwaseba Alisema muda mfupi baada ya Timu hiyo kuwasili kuwa Timu iko salama na Wameanza mazoezi mepesi kwa Ajili ya Kujiandaa na Michuano hiyo sambamba na kuzoea hali ya hewa.

“Timun yetu iko vizuri kilizhobaki watanzania waendelee kuiombea Timu yetu kwani maombi yao yakichanganyika na jitihada za Timu basi ushindi utapatikana na ni vema Watanzania walioko Rwanda kujitokeza kushangilia Timu zao,Alisema Brigedia Jenerali mwaseba.

Wakati huo huo Mkuu wa majeshi wa Rwanda Jenerali Patrick Nyamvumba akizungumza Na Waandishi wa Habari alisema Maandalizi yote yamekamilika na kinachosubiriwa ni kuanza kwa Michezo hiyo huku Timu zikimalizia hatua za Mwisho za Usajili kwa ajili ya Michuano hiyo

Alisema Wanajeshi 500 kutoka katika Majeshi ya Nchi Nne za Tanzania,Rwanda,Uganda, na Kenya wanatarajiwa kushiriiki katika Mashindano ya Kumi ya Majeshi ya Nchi za Afrika Mashariki huku Burundi ikiwa imeshindwa kushiriki kutokana na hali ilivyo katika Nchi yake.

Jenerali Nyamvumba alisema anamatumani makubwa na mazungumzo yanayoendelea kuhusu Burundi hivyo Matarajio yake yataifikisha Burundi katika Hatua Nzuri na Hivyo kushiriki katika Michezo hiyo ambayo aliita Muhumi kwa Ushirikiano.

“Michezo hii ni Muhimu kwa Ushirikiano wetu kwani hakuna Mshindi mwisho wa mashindano sote tunakuwa washindi kutokan na kufanikisha kuwa pamoja,Urafiki kama kamajeshi yaliyo katika Ukanda wa Afrika Mashariki,” Alisema Jenerali Nyamvumba.

Kwa Upande Wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi kutoka Tanzania Brigedia Jenerali Martin Kemwanga amesema kama kamati waliridhia kuwepo kwa Michezo Mitano ambayo ni Mpira wa miguu,Kikapu,Pete,Mikono na Mbio za Nyika.
Mkuu wa Majeshi ya Rwanda (CDS) Jenerali Patrick Nyamvumba (Kushoto)akiongea na Waandishi habari Hawapo Pichani katika Ukumbi wa Uwanja wa Amahoro Juu ya maandalizi ya mashindano ya majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki yanayotarajia kufungulia Kesho(Leo Jumatatu Agosti 8)Kulia ni Mwenyekiti wa kamati ya Mandalizi Brigedia Jenerali martin Kemwanga wa JWTZ.
Mwenyekiti wa kamati ya Mandalizi ya Mashindano ya 10 ya Majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki Brigedia Jenerali Martin Kemwanga wa JWTZ akifafanua jambo Mbele ya Waandishi wa habari (Hawapo Pichani)Mjini Kigali kuhusu Maandalizi ya mashindano hayo kushoto ni Mkuu wa Majeshi wa Rwanda (CDS) Jenerali Patrick Nyamvuba ).
Baadhi ya Viongozi na Wachezaji wa Timu za Jeshi wanaoshikiri Michuano ya Kumi ya Majeshi kwa Nchi za Afrika mashariki yanayotaraji kufunguliwa Kesho (Leo) katika Uwanja Wa Amahoro Mara walipowasili katika Mji wa KigalI Nchini Rwanda .(Picha na Selemani Semunyu).

KATIBU MKUU MALIASILI NA UTALII AONGOZA WATUMISHI WA WIZARA HIYO KUMUAGA ALIYEKUWA MKURUGENZI WA UTAWALA NA RASILIMALI WATU, SAID MSAMBACHI

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Maj. Gen. Gaudence Milanzi (kushoto) akizungumza katika hafla fupi iliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Utumishi, Said Msambachi (kulia) aliyestaafu rasmi kwa mujibu wa sheria tarehe 16 Juni, 2016. Hafla hiyo ilifanyika juzi tarehe 05 Agosti, 2016 katika ukumbi wa mikutano wa Selous, Makao Makuu wa Wizara hiyo, Jengo la Mpingo, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi (kulia) akitoa nasaha zake kwa watumishi wa Wizara hiyo katika hafla fupi ya kumuaga iliyoandaliwa na watumishi hao tarehe 05 Agosti, 2016. Aliwaasa watumishi hao kutekeleza majukumu yao kwa kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na uaminifu kama chachu ya maendeleo yao kazini. Aliwataka pia kufanya kazi kwa ushirikiano kujiepusha na majungu, vitendo vya rushwa na ubaguzi pahala pa kazi. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maj. Gen. Gaudence Milanzi.
Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Said Msambachi na Mama Msambachi wakikata Keki ya kuagwa waliyoandaliwa na watumishi wa Wizara hiyo.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

MATARUMA YA KIWANDA CHA KONGOLO CHA TAZARA-MBEYA KUJENGA RELI YA KISASA.

Serikali imesema itatumia kiwanda cha Kongolo cha Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) kilichopo Mbeya kuzalisha mataruma yatakayotumika kwenye ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) inayotarajiwa kuanza kujengwa hivi karibuni ili kupunguza gharama.

Hayo ameyasema Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa alipotembelea kiwanda hicho kuona utendaji kazi na  uzalishaji unaopatikana na kuiagiza kamati maalumu ya ujenzi wa reli hiyo kutembelea kiwandani hapo kuangalia uwezo wa uzalishaji wa kiwanda hicho.

Profesa Mbarawa amesema Serikali ina dhamira ya kufufua viwanda hapa nchini ili kuongeza fursa za ajira kwa Watanzania na kuifikisha nchi katika uchumi wa kati kupitia mapinduzi ya viwanda ifikapo mwaka 2025.

"Nitahakikisha mkandarasi atakeyejenga reli hii anatumia mataruma yatakayozalishwa katika  kiwanda hiki, badala ya kuagiza vifaa vya ujenzi kutoka nchi za nje", amesema Waziri Prof. Mbarawa.

Ameongeza kuwa kwa kutumia kiwanda hicho Serikali itaokoa pesa ambazo zitaisaidia TAZARA kujiongezea mapato yatakayotokana na matengenezo ya mataruma na kupanua wigo wa kibiashara kwa wateja wa ndani na nje ya nchi.

Aidha, Waziri Prof. Mbarawa amekagua maabara ya kupima viwango na ubora wa kokoto na nondo kilichopo kiwandani hapo na kutoa mwezi mmoja  kwa TAZARA kupata cheti cha ukaguzi kutoka Shirika La Viwango (TBS), ili iweze kurasimishwa rasmi.

Kwa upande wake Msimamizi Mkuu wa kuzalisha mataruma katika Kiwanda Cha Kongolo cha TAZARA-Mbeya Eng. Boniface Phiri amesema kuwa fursa ya kuwa sehemu ya mradi wa ujenzi wa reli ya Kisasa itaongeza uzalishaji wa kiwanda na kukuza pato la Mamlaka. "Kwa kushirikiana na wenzetu tutaongeza vifaa ili tuweze kuzalisha kwa wingi na ubora unaotakiwa katika mradi huu", amesema Eng. Phiri.

Kiwanda cha Kongolo ni kiwanda pekee katika nchi za Afrika na kati kinachozalisha mataruma kwa ajili ya reli na kina uwezo wa kuzalisha mataruma elfu ishirini na  nne kwa mwaka. Waziri Prof. Mbarawa yupo katika ziara ya kukagua miundombinu ya reli, barabara na mawasiliano mkoani Mbeya.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa(Kushoto) akitoa maelekezo kwa Afisa Mfawidhi Kutoka Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) Bw.Denis Daudi, wakati alipokagua huduma za mabasi katika kituo cha nane nane Mkoani Mbeya.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa pili Kushoto), akikagua moja ya kifaa kinachotumika kwenye Reli wakati alipotembelea kiwanda cha Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia(TAZARA), Kongoro Qwarre kilichopo Mkoani Mbeya.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wa tatu kushoto) akikata moja ya kifaa kinachotumika kujengea reli wakati alipotembelea kiwanda cha Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia, Kongoro Qwarre kilichopo Mkoani Mbeya.


HALMASHAURI YA IKUNGI YAPATIWA ZAIDI YA SHILINGI MIL. 900 KUJENGA DARAJA LA MINYUGHE

SERIKALI imeipatia Halmashauri ya wilaya ya Ikungi, Mkoani Singida zaidi ya shilingi milioni mia tisa kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa daraja la mto Saiwa, uliopo katika Kijiji cha Minyughe, tarafa ya Ihanja,wilayani Ikungi ili kuwanusuru wananchi wa vijiji vya Minyughe, Majengo, Mayaha, Mtavira na Mteva wasipoteze maisha yao kwa kusombwa na maji yanayosafiri kupitia mto huo.

Kukosekana kwa daraja hilo kwa zaidi ya miaka kumi sasa kumechangia watu na mifugo kupoteza maisha, magari kusombwa na maji yanayosafiri kupitia kwenye mto huo.

Akizungumza na wananchi wa vijiji vya Minyughe na Misake, tarafa ya Ihanja, wilayani hapa, Mbunge wa jimbo la Singida magharibi, Elibariki Kingu aliweka bayana kwamba gari moja la Kampuni ya vinywaji baridi la Pepsi, lilizama na kisha kudidimia kwenye mchanga ambapo mpaka leo halijaweza kutolewa.
Mmoja wa wananchi wanaosafirisha mizigo yao kwa kutumia usafiri wa baiskeli akijaribu kuvuka katika eneo la mto huo ambao kwa sasa umekauka kama alivyonaswa na kamera ya mwandishi wa wetu.

Mbunge huyo ambaye alikuwa katika ziara ya kutembelea na kukagua ujenzi wa daraja hilo iwapo Mkandarasi wake ameanza shughuli za ujenzi wa daraja hilo.

Kwa upande wake Mhandisi wa ujenzi wa Halmashauri hiyo,Haruna Mbegalo licha ya kukiri Halmashauri ya wilaya hiyo kupokea fedha za ujenzi wa daraja hilo,lakini alitofautiana na Mbunge huyo kwa kudai kuwa Halmashauri hiyo imepokea zaidi ya shilingi milioni mia saba kwa ajili ya shughuli hizo.

“Tatizo la mto Minyughe au mto saiwa tunalishughulikia, Mkandarasi ameshapatikana,ameshaonyeshwa site na ameanza zile taratibu za awali na sasa hivi alikuwa anasubiri maji yapungue au mto ukauke ili aweze kuanza shughuli za ujenzi”alifafanua Mhandisi Mbegalo.
Kwa mujibu wa Mhandisi huyo kiasi hicho cha zaidi ya shilingi milioni mia saba zilitengwa katika kipindi cha mwaka wa fedha uliopita wa 2015/2016 na kwamba shughuli za ujenzi huo zimekwishaanza kwa kufanyika kwa upembuzi yakinifu ambapo mpaka sasa zaidi ya shilingi milioni 103 zimetumika.

Hata hivyo akizungumzia suala la fidia kwa wananchi waliokuwa wakiishi kuzunguka eneo la mto huo wanaotakiwa kuhama kupisha mradi huo,Mhandisi Mbegalo alikiri kuwa hakuna fedha zozote zilizotengwa kwa ajili ya kuwalipa wananchi hao.

Wakizungumzia madhara yaliyopatikana na ambayo endapo daraja hilo halitajengwa yataendelea kutokea,baadhi ya wananchi wa Vijiji hivyo waliyataja kuwa ni pamoja na kukwama kwa magari ya abiria na mizigo pamoja na binadamu na mifugo kupelekwa na maji yanayopita kwenye mto huo.

Katika kipindi cha kuanzia mwaka 2015 hadi sasa zaidi ya magari ya mizigo 15,mabasi ya abiria 5,wanyama wafugwao zaidi ya 50 walisombwa na maji huku magari yakizama kwenda chini ya maji na kushindikana kuvutwa.
Muonekano wa sasa ukiwa umekauka mto Saiwa uliopo katika Kijiji cha Minyughe,Tarafa ya Ihanja,wilaya ya Ikungi,Mkoani Singida ambao ni tishio kwa watu wanaopia katikati ya mto, magari ya mizigo, magari ya abiria pamoja na mifugo inayokwenda kunywa maji.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Minyughe,tarafa ya Ihanja waliokutwa wakinywa maji kwenye mto Saiwa walipokuwa wakirudi kutoka shuleni wakienda nyumbani baada ya masomo yao ya asubuhi.(Picha zote Na.Jumbe Ismailly).

UCHAMBUZI WA MAGAZETI LEO


SERENGETI BOYS ILIVYOWADINDIA WASAUZI

Ikicheza mbele ya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na Naibu Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Rosemary Chambe Jairo, timu ya soka ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 maarufu kama Serengeti Boys leo imegoma kupoteza mchezo dhidi ya wenyeji Afrika Kusini baada ya kuibana Amajimbos na kutoka sare bya bao 1-1.

Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Dobsonville ulioko Soweto, Mji ulioko Kusini –Magharibi mwa jiji la Johannesburg, mabao yote yalipatikana kipindi cha pili yakiwa ni ya penalti kwa kila upande. Afrika Kusini walianza kupata penalti katika dakika 65 iliyofungwa na Linamandlia Mchilizeli kabla ya Ally Msingi kuisawazishia Serengeti Boys katika dakika ya 70.

Penalti ya Afrika Kusini ilitokana na mmoja wa mabeki wa Serengeti Boys kumfanyia madhambi Mchilizeli  wa Amajimbos ndani ya eneo la hatari wakati ile ya Serengeti Boys ilitoakana na beki Luke Donn wa Amajimbos kunawa mpira eneo la hatari.

Afrika Kusini iliyoanza kwa kasi dakika 10 za mwanzo wa mchezo huo, ilipotea dakika zote 30 za kipindi cha kwanza ambao kukosa bahati na umakini kidogo tu kwa nyota wa Serengeti Boys kulisababisha kukosa mabao matano yakiwamo mawili yaliyogonga mwamba hivyo kuwatia hasira Serengeti Boys ambao walionyesha kuwa na njaa ya mabao.

Kubanwa katika kipindi cha kwanza, kulisababisha Kocha Mkuu wa Amajimbos kufanya mabadiliko ya wachezaji wote watatu kipindi cha pili, wakati Bakari Shime kwa upande wake alimpumzisha Ibrahim na nafasi yake kuchukuliwa na Muhsin ambaye alisaidia kuendedlea kuwabana Afrika Kusini waliokjuwa wanawategemea nyota kama na Mswati Mavuso na Lethabo Mazibuko.
Shukrani za pekee zinaweza kwenda kwa Kipa Ramadhani Kabwili aliyeokoa hatari nyingi ikiwamo mpira uliokuwa unakwenda golini uliotokana na adhabu ndogo. Kadhalika Msengi aliyekuwa nyota wa mchezo huo akimiliki vema idarta ya ulinzi akishirikiaana nDickson Job.

Shime maarufu kama Mchawi Mweusi alisema: “Nashukuru kwa matokeo haya. Si mabaya kwangu. Tunarudi nyumbani kujipanga. Afrika Kusini ilikuwa inanitia hofu ndio maana nilisema mechi itakuwa ngumu.”

Kwa upande wake, Naibu Balozi Rosemary alisema: “Ahsanteni vijana (Serengeti Boys) kwa kulinda heshima yangu,” wakati Malinzi alisema: “Sina mengi. Mkiwafunga Afrika Kusini Agosti 21, 2016 kambi inapigwa tena nje ya nchi. Sijui ni nchi gani, lakini mtakwenda kujiandaa nje ya nchi.”

Katika mchezo huo, Kikosi cha Serengeti kilikuwa: Ramadhani Kbawili, Israel Mwenda, Nickson Kibabage, Ally Msengi, Dickson Job, Shaban Ada, Kelvin Naftal, Ally Ng’anzi, Ibrahim Abdallah/Muhsin Makame (Dakika ya 72), Asad Juma na Mohammed Rashid.

Afrika Kusini: Glen Tumelo, Mswati Mavuso, Luke Donn, Sechaba Makoena, Kwenzokuhle Shinga, Mjabulise Mkhize, Bonga Dladla, Linamandla Mchilizeli, Luke Gareth, James Monyane na Siphamandla Ntuli.

FRIEDKIN CONSERVATION FUND NA AFRICAN WILDLIFE TRUST WADHAMINI ROCK CITY MARATHON


IKIWA ni sehemu ya mkakati wa kupambana na ujangili pamoja na kutangaza utalii wa ndani kampuni za Uhifadhi za Friedkin Conservation Fund (FCF) na African Wildlife Trust (AWT) zimeamua kudhamini Rock City Marathon inayotarajiwa kufanyika Septemba 25 kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana kuhusiana na udhamini huo wa miaka mitatu, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hizo Bw Pratik Patel alisema kampuni mzake zitatumia mbio hizo kuzindua kampeni yao inayofahamika “*Okoa Wanyama Wetu*; *Kataa Ujangili”*

“Tutatumia Rock City Marathon kutangaza kampeni yetu ya kupinga ujangili
itakayofanyika katika baadhi ya majiji ulimwenguni.,’’ alibainisha Pratik. Alisema kampeni hiyo ya “*Okoa Wanyama Wetu*; *Kataa Ujangili”* itaanza nanmatembezi yatakayofanyika Septemba 24 mwaka huu jijini Arusha, Moshi na Dar es Salaam yakifuatiwa na mbio hizo Septemba 25, Uwanja wa CCM Kirumba.

“Tuliamua kudhamini Rock City Maratahon kwa kuwa lengo la mbio hizi ni
kutangaza utalii wa ndani na sisi tuliona kwamba huo utalii unaotangazwa
ili uwe na tija zaidi unategemea uwepo wa maliasili. Na ni wazi kwamba
uwepo wa maliasili hizi unategemea sana jitihada za kweli katika uhifadhi
wake! Na hapo ndipo hasa utatukuta sisi ,’’ alisema.

Wakizungumza kwenye uzinduzi wa mbio hizo jijini Mwanza hivi karibuni, Mkuu wa mkoa huo John Mongella na Mkuu wa mkoa wa Simiyu ambae pia ni Rais wa chama cha riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka walipongeza wadhamini wa mbio hizo zikiwemo kampuni za Friedkin Conservation Fund (FCF) na African Wildlife Trust (AWT) kwa kuunga mkono jitahada za serikali  katika kutangaza utalii wa ndani pamoja na kupambana na ujangili hapa nchini.

Pamoja na pongezi hizo pia viongozi hao wa walikuwa wa kwanza kujisajili
kushiriki Rock City Marathon huku wakiahidi kuhakikisha kwamba mbio
zinapata washiriki wa kutosha sambamba na wadhamini kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Mbali na kampuni za Freidkin Conservation Fund na African Wildlife
Trust,wadhamini wengine wa mbio hizo ni pamoja na  Mwanza Hotel, Nyanza Bottlers Limited, Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Real PR
Solutions na kampuni ya Fabec.

Akizungumzia mbio hizo Mratibu kutoka kampuni ya Capital Plus Bw Mathew Kasonta alisema Rock City Marathon zitahusisha makundi matano yaani mbio za kilomita 21 kwa wanaume na wanawake, kilomita 5 kwa ngazi ya ‘corporate’, kilomita 3 kwa ajili ya walemavu na zile za wazee umri zaidi miaka 55 na kuendelea pamoja na kilomita 2 kwa ajili ya watoto umri kati ya miaka 7 hadi 19.

Pia litoa wito kwa wakazi wa jiji la Mwanza na mikoa jirani kujisajili kwa
kuchukua fomu katika vituo kadhaa vikiwemo Ofisi za michezo wilaya zote za
mkoa wa Mwanza, Ofisi zote za riadha mikoa ya Geita, Simiyu na
Shinyanga,   Uwanja wa Nyamagana,  Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino  Mwanza, Kituo cha michezo Malya na Shule ya Kimataifa ya Isamilo,

“Kwa upande wa Dar es Salaam Fomu za ushiriki pia zinapatikana katika ofisi za Kampuni ya Capital Plus International zilizopo ghorofa ya tatu jengo la ATC, jijini Dar es, Salaam na vituo vingine vitaendelea kutangazwa hivi
karibuni,” alihitimisha.

SERIKALI YA BRAZIL YAONYESHA NIA YA KUFANIKISHA AZMA YA RAIS. DKT. MAGUFULI KUIFANYA TANZANIA KUWA NCHI YA VIWANDA

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Brazil nchini Tanzania, Carlos Alfonso Puente, wakati Balozi huyo alipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Balozi wa Brazil nchini Tanzania, Carlos Alfonso Puente (Kushoto), akisaini Kitabu cha Wageni ofisini kwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Kulia), alipomtembelea Waziri na kufanya naye mazungumzo kuhusu ushirikiano baina ya nchi hizo mbili hususan katika uwekezaji kwenye sekta ya nishati.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Kushoto), akimsikiliza kwa makini Balozi wa Brazil nchini Tanzania, Carlos Alfonso Puente (Kulia), wakati Balozi huyo alipomtembelea Waziri Ofisini kwake jijini Dar es Salaam hivi karibuni na kufanya mazungumzo naye kuhusu masuala ya uwekezaji katika sekta za nishati na madini. Wengine pichani ni Maafisa wa Wizara waliohudhuria mkutano huo.

Na Veronica Simba

Serikali ya Brazil imeonesha nia kuwekeza katika sekta ya nishati nchini hususan katika kuzalisha umeme kwa kutumia maji na mabaki ya miwa. Hayo yameelezwa jana jijini Dar es Salaam na Balozi wa Brazil nchini Tanzania, Carlos Alfonso Puente, alipomtembelea Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo ofisini kwake na kufanya mazungumzo naye.

Balozi Puente alimweleza Profesa Muhongo kuwa nchi yake inao ujuzi na uzoefu wa kutosha katika uzalishaji wa umeme kwa kutumia vyanzo mbalimbali hususan maji.

Alisema, Brazil ingependa kuchangia kufanikisha azma ya Rais John Magufuli kuifanya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda.

“Kutekeleza mchakato wa kuifanya nchi kuwa ya Viwanda, unahitaji umeme mwingi unaotokana na vyanzo mbalimbali. Ni bahati nzuri kwamba Tanzania inazo njia za kufanikisha azma hiyo,” alisema.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

No comments:

Post a Comment